SIMBA YA MAMILIONI ILIVYOMSHANGAZA SURE BOY.
BAADA ya kutoka suluhu na Simba, kiungo mshambuliaji
wa Azam FC, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, amefunguka
licha ya usajili wa Simba kutumia mabilioni ya shilingi
lakini timu hiyo imekuwa na uwezo mdogo uwanjani.
Simba inatajwa kutumia jumla ya Sh bilioni 1.3 katika
usajili wake wa msimu huu na kupelekea kuwa kikosi
ghali zaidi kikiwa na mastaa mbalimbali akiwemo
Emmanuel Okwi, John Bocco na Haruna Niyonzima.
Sure Boy ameyasema hayo kufuatia kutoka sare ya
bila kufungana na timu hiyo katika mchezo wa
Ligi Kuu Bara uliopigwa juzi Jumamosi kwenye
Uwanja wa Azam Complex ulipo Chamazi nje kidogo la Jiji la Dar.
Akizungumza nasi Sure Boy alisema kuwa
hakutarajia wapinzani wao kucheza katika
kiwango cha kawaida kama ilivyotokea kwa
kuwa wana timu inayodaiwa kusajiliwa kwa pesa nyingi.
“Mechi haikuwa rahisi na wala haikuwa ngumu
sana ila tunashukuru kwa matokeo ambayo
yametokea, tulijipanga kushinda mchezo wa leo (juzi)
lakini haikuwa bahati kwa sababu ukiangalia sisi
ndiyo tulikuwa bora zaidi ya wenzetu na tulistahili kushinda.
“Simba naweza kusema imecheza kwenye kiwango
cha kawaida sana kwa sababu tumemiliki mpira
na kufanya mashambulizi ya maana zaidi yao,
ndiyo maana nasema ya kawaida kwani imekuwa
tofauti na thamani yake inayosemwa,”alisema Sure Boy.
No comments