SHAIRI: HUYU NDIYE MREMBO WA UDSM "PASUA KICHWA"
SALOME WA UDSM
SHAABAN MAULIDI
TABORA TANZANIA
Jina lake ni Salome, bint wa mzee Lyimo,
Kitabu changu nisome, yeye
kwangu kama somo,
Shahidi Sam Kameme, kweli
yaliyomo yamo,
Uwapi wangu Salome, basi rudi UDSM.
Wa Arusha siyo Tanga, mimi
wake Sweet Mangi,
Mbalamwezi yake mwanga, pink
ndiyo yake rangi,
Ananyonga ni kinyonga, kama ringi yeye haringi,
Uwapi wangu Salome, basi rudi UDSM.
Zimenoga zake lipsi, zimenona
zake Hipsi,
Anang'ara kama Chipsi, ni
mtamu kama Pepsi,
Mashavuni ana Dimpsi, chuchu
zake kama Tipsi,
Uwapi wangu Salome, basi rudi UDSM.
Nilikwona tu kwa Sago, sikukwona
kwa Sumbay,
Sketi zako za mitego, kumshinda
hata Ney,
Hutumii mikorogo, kama ya
Kigosi Ray,
Uwapi wangu Salome, basi rudi UDSM.
Nkamuliza Antonia, mpaka
kaka Kamili,
Nkamuliza Sofia, na rafiki yako Lili,
Semina za Historia, na
lekcha za Kiswahili,
Uwapi Wangu Salome, basi
Rudi UDSM.
Ndo upo kwa Diamond, kuimbwa
na Rayvani,
Au ndo kwa Mau_Fund, Maufundi
kitandani
Ama Eric Omond, Sang'ombe ndo jina gani?
Au kwa Yamoto Band, wakupwelepweta
ndani,
Uwapi Wangu Salome, basi
Rudi UDSM
.
Jina langu Shaabani, ukipenda
Maulidi,
Wewe kwangu ni kidani, cha
dhahabu ndo zawadi,
Maua kwenye bustani, nakuchuma
we waridi,
Kipimo chako wastani, siyo
joto si baridi,
Uwapi Wangu Salome, basi
Rudi UDSM.
Mwisho natuma salamu, uishi
maisha mema,
Bado kwako nina hamu, uwe
wangu mke mwema,
Nikupende kwa nidhamu, nikupeleke
kwa mama,
Uwapi Wangu Salome, basi
Rudi UDSM.
Itaendelea..
Na Shablil President
Wa Nyamwezi Kingdom
2017 Kamilisha Malengo
0718526159/0718526159
No comments