Header Ads

HII NDIYO SABABU YA RAIS MAGUFULI KUMTEUA KAIMU JAJI MKUU















Rais John Magufuli amefichua
 siri ya kumteua Profesa 
Ibrahim Juma kuwa Kaimu
 Jaji Mkuu akisema hakuwa 
na historia ya kutosha ya 
majaji wengi alipoingia madarakani.

Amesema alipoingia madaraka
 ilikuwa kipindi kifupi ambacho 
aliyekuwa Jaji Mkuu, 
Mohamed Chande Othman
 alistaafu hivyo ilimlazimu
 achukue muda mrefu wa
 kujiridhisha na alitumia
 Ibara ya 118 (4) kumteua Kaimu Jaji Mkuu.

Rais Magufuli amesema 
hayo leo Jumatatu, Ikulu jijini 
Dar es Salaam wakati wa 
kumwapisha Jaji Mkuu,
 Profesa Juma baada ya 
kumteua jana Jumapili.

Hafla hiyo imehudhuriwa na
 viongozi mbalimbali akiwemo 
Makamu wa Rais, Samia 
Suluhu Hassan na Waziri 
Mkuu, Kassim Majaliwa.

“Nilifanya hivi si kwa sababu 
hakuna majaji au walikuwa 
hawafai, majaji wote ni 
wazuri na mnafanya kazi
 nzuri sana lakini sikutaka
 kuteua jaji baada ya mwaka
 mmoja nateua tena au 
baada ya miaka miwili anastaafu,
 nilitaka nikiteua akae miaka
 hata 10, awe ‘anatujaji’ wote 
tutakaokuwepo,” amesema Rais Magufuli.

Amesema kumteua Jaji Mkuu 
ni kazi ngumu, lazima ujue historia
 na tabia zake, pia kuangalia iwapo
 ataweza kuendana na dhamira 
yake ya kupambana na rushwa.

Rais Magufuli amesema rushwa
 ipo kila sehemu, hivyo baada
 ya kuchaguliwa na wananchi
 mwaka 2015 alikaa chini 
na kumwomba Mungu apate
 kiongozi atakayeenda kulisimamia
 jambo hilo kwa kipindi kirefu zaidi.

Amesema wapo majaji wengi 
na wenye sifa lakini baadhi yao
 wamebakisha muda mchache kustaafu.

“Katika kufanya uchambuzi 
wangu nikamwona Profesa 
Juma ambaye alikidhi vigezo
 vyangu. Nakupongeza s
ana Profesa Juma ni 
Mungu ambaye amekuchagua 
kwa hiyo, kawatumikie vizuri 
watu wa Mungu na utangulize
 mbele masilahi ya Watanzania,” amesema.

Rais Magufuli amesema ingawa 
bado kuna changamoto mbalimbali
 katika Mhimili huo, alimuhakikishia 
Profesa Juma kwamba Serikali
 inazitambua na aliwataka majaji 
kutembea kifua mbele kwa 
kuwa Serikali inatambua kazi 
nzuri wanayoifanya.

Amesema kazi nzuri yoyote
 haikosi watu wa kuiponda, 
akitumia msemo wa mti 
wenye matunda ndiyo 
unaopopolewa kwa mawe.

Kiongozi huyo mkuu wa 
nchi amesema alipomteua
 kuwa Kaimu Jaji alipondwa 
lakini alikuwa mvumilivu na
 hakupata shinikizo la mtu
 yeyote la kumteua Jaji Mkuu.

No comments

Powered by Blogger.