MANJI ASEMA YEYE BADO NI DIWANI AKIWA MAHAKAMA
MFANYABIASHARA Yusuf Manji
ameieleza Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu leo September 9, 2017
kuwa yeye bado ni Diwani wa Kata ya
Mbagala Kuu na kudai kuwa hatambui
kuvuliwa udiwani kama ilivyotangazwa
na Mstahiki Meya wa Temeke,
Abdallah Chaulembo September 6, 2017.
Manji ametoa malalamiko hayo, kwenye kesi
ya uhujumu uchumi inayomkabili na wenzake
mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma
Shaidi ambapo katika kesi hiyo ambayo
Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa
Kishenyi amedai upelelezi haujakamilika na
Manji kudai ameona habari kupitia gazetini
kuwa amevuliwa udiwani.
Amedai kama ni kweli amevuliwa Udiwani
hatambui, kwani ana miezi 2 yupo gerezan
i na serikali inatambua kwamba yeye ni Diwani.
“Vikao vya awali vya udiwani wa Halmashauri
ya Temeke nilikuwa nahudhuria kwa kuwa
naheshimu Mahakama na kwa uzito wa hii
kesi sikutaka kupeleka hata maombi y
a dhamana Mahakamani.
“Mahakama imuagizie DPP na aiambie
Halmashauri ya Temeke kwamba
wamenikamata na ndio sababu
ya kutohudhuria vikao. Kama wanataka
nihudhurie DPP aombe remove order
nitolewe gerezani ili niende kwenye vikao.”
Pia Manji amedai kuwa kama hilo
haliwezekani, basi wamuandikie
barua itakayoonyesha agenda
ya vikao vyote na yeye atazijibu
kwa njia ya barua pia.
“Ninachotambua mimi ni Diwani
wa Mbagala Kuu na kama
nimevuliwa au sijavuliwa
udiwani sitambui. Tayari nimetumia
fedha zangu mwenyewe zaidi ya
Tsh. Milioni 70 sio za Halmashauri
kwa ajili maendeleo ya wananchi wake.”
Aidha, amedai kuwa hiyo kesi ni nzito
na DPP hapaswi kuangalia upand
e wake wa kesi tu, kwani yeye
amechaguliwa na wananchi na anawasaidia.
Awali kabla ya kuelezwa hayo, Wakili
wa utetezi Seni Malimi alidai kuwa
wanatarajia kuwasilisha maombi
ambayo ni ya siri katika tarehe ijayo.
Baada ya kuelezwa hayo, Hakimu
Huruma Shaidi akautaka upande
wa mashtaka kuhakikisha
wanalifanyia kazi suala hilo
, ambapo kesi imeahirishwa
hadi September 18, 2017.
No comments