JEZI YA TSHISHIMBI YAWA LULU
tayari zimeanza kuuzwa kwa kiwango cha juu
mkoani Njombe ikiwa ni siku chache kabla
ya Yanga haijacheza na Njombe Mji
kwenye Uwanja wa Sabasaba mkoani humo.
Njombe Mji na Yanga zinatarajiwa kupambana
keshokutwa Jumapili ukiwa ni mchezo wa
Ligi Kuu Bara ambapo Tshishimbi tayari
ameshajizolea umaarufu kutokana na
kiwango kikubwa alichokionyesha
kwenye mechi yake ya kwanza hapa
nchini dhidi ya Simba katika Ngao ya Jamii.
Jana Alhamisi, tulizipata picha
mbalimbali zikionyesha
wafanyabiashara wa jezi
katika Stendi Kuu ya Mabasi Njombe.
Licha ya kuwepo kwa jezi nying
i za wachezaji mbalimbali wa
Yanga, lakini zenye jina la
Tshishimbi raia wa DR Congo,
ndizo zilikuwa nyingi huku
ikisemekana kwamba ndizo
zilizokuwa zikinunuliwa kwa wingi.
No comments