NIYONZIMA AFUNGUKA JINSI SIMBA ITAKAVYOBEBA UBINGWA MSIMU HUU
KIUNGO wa Rwanda na Simba, Haruna
Niyonzima, amesema moja ya maleng
o aliyojiwekea ni kuhakikisha timu hiyo
inatwaa ubingwa wa Kombe la Shirikisho
Afrika hapo mwakani.Simba ilikata tiketi
ya kushiriki michuano yaKombe la Shirikisho
Afrika baada ya kuibuka mabingwa wa Kombe
la FA msimu uliopita
Kiungo huyo aliyejiunga na Simba msimu
huu akitokea Yanga, alisema ubora wa
kikosi chao ndio unaomfanya aamini
wana kila sababu ya kubeba taji hilo.
“Simba tuna kikosi bora msimu huu ndiyo
maana nawaza ubingwa wa Afrika, naamini
inawezekana kwa sababu ya aina ya
wachezaji na kama tutajituma hakuna
kitakachoshindikana,” alisema Niyonzima.
Niyonzima alisema licha ya ubora
wa kikosicha Simba kwa sasa,
anaamini yeye binafsi ana bahati
ya kuzipa mafanikio timu mbalimbali
alizowahi kuzichezea tangu akiwa
nchini kwao Rwanda na baada ya
kutua Tanzania.Alisema anatambua
haitakuwa kazi rahisi, lakini kiu ya
mafanikio waliyokuwa nayo msimu
huu anaamini itawasaidia kufikia
malengo.Hata hivyo, pamoja na
kuichezea timu yake ya zamani ya
Yanga kwa miaka mitano, Niyonzima
hakuwahi kufanikiwa kutwaa
ubingwa wowote wa michuano ya Caf.
No comments