MCHEZAJI BORA WA LIGI AKAA BENCHI MECHI MBILI MFULULIZO
AMA kweli hakuna ufalme unaodumu milele!
Beki Mohammed Hussein ‘Tshabalala’
alikuwa kama mfalme wa nafasi ya
kushoto msimu uliopita pale Simba na
aliweka rekodi ya kucheza mechi zote
za ligi, lakini mambo yamebadilika msimu
huu, amepata mpinzani na amepigwa
benchi mechi mbili mfululizo kwenye ligi.
Juzi Simba ilicheza dhidi ya Azam FC
kwenye Uwanja wa Azam Complex,
Chamazi jijini Dar na kutoka suluhu.
Tshabalala alikuwa benchi.
Tshabalala hadi sasa ameshindwa kufua
dafu mbele ya beki mpya wa timu hiyo,
Erasto Nyoni ambaye amejiunga na
klabu hiyo hivi karibuni akitokea Azam FC.
Kocha Mkuu wa Simba, Mcameroon,
Joseph Omog amekuwa akimpatia Nyoni
nafasi ya kucheza kila wakati kutokana na
kuonyesha uwezo mkubwa tangu alipojiunga
na timu hiyo.
Akimzungumzia mchezaji huo, Omog alisema:
“Nyoni ni mchezaji mwenye faida kubwa anapokuwa
uwanjani, mbali ya kucheza nafasi ya beki wa
kushoto lakini pia ana msaada mkubwa kwa mabeki
wa kati na pindi tunapokuwa tunashambuliwa.
“Anajua kukaba vizuri lakini pia anajua kuanzisha
mashambulizi, kwa hiyo ni mtu muhimu sana katika kikosi changu.
“Kuhusu Tshabalala ni mchezaji mzuri lakini siwezi
kuwatumia wote kwa pamoja ila atacheza tu, mechi bado ni nyingi.”
No comments