VIJANA CHANGAMKIENI FURSA – MAVUNDE
Naibu Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,
Bunge, Kazi,Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu
Mh.Anthony Mavunde jana alikuwa mgeni
rasmi katika uzinduzi rasmi msimu wa
FURSA 2017 mkoani Arusha.
“Tumehutubia sana,tumesema sana, tumejadili
sana,tumepanga mipango sana, sasa ni wakati
wa kuachana na dhana hii na kutenda, kufanya,
na sio kufanya tu bali kufanya kweli” ..
Ni maneno alionena kwa hisia kali Naibu Waziri
Ni maneno alionena kwa hisia kali Naibu Waziri
Anthony Mavunde akizungumza na mamia ya
vijana na vikundi mbalimbali mkoani Arusha
Tanzania katika muendelezo wa msimu wa
FURSA 2017.
Naibu Waziri Mavunde aliwataka Vijana
kuhakikisha wanatumia fursa ya Mifuko 19
ya Uwezeshwaji Wananchi Kiuchumi kama
sehemu ya kupatia mitaji ya shughuli
mbalimbali za kiuchumi na hivyo kusaidia
kuondokana na masharti magumu ya
Taasisi za Fedha nyingi.
Aidha pia, Aliwashukuru sana timu nzima
ya Fursa chini ya muasisi ndg.Ruge Mutahaba
kwa kuzidi kuisaidia jamii ya kitanzania na
serikali kwa ujumla wake kufanikisha maendeleo
ya nchi hii na kuonesha kwa vitendo dhana nzima ya ushirikishwaji.
Mgeni Rasmi ndugu Mavunde aliizungumzia
dhana hii ya Fursa na kauli mbiu yake mwaka
huu ya Anzia Sokoni akiwataka vijana na
watanzania wote wanaotaka kufanikiwa
kutokata tamaa na kuwa na malengo
yenye tija, kuhakikisha kila siku wanaitumia
kuwaza jambo la kufanya na la kuwaletea maendeleo.
Pia,alizungumza ni namna gani serikali mpaka
sasa imefanya katika kuhakikisha ina watengenezea
vijana mazingira bora na kukazania kwenye mipango
iliyopo kwao kuanzia wale walio katika mfumo rasmi
wa elimu na wale walionje ya mfumo kuwatengenezea
mazingira ya kuendeleza shughuli zao mfan
o useremala,ushonaji nk kuwapa mafunzo na kuwatengeneza kua bora.
Mwisho aliwashukuru washriki wa Fursa 2017 Umoja wa
mataifa kwa kuendelea kushika ajenda hii ya vijana ikiwa
kwa mkoa wa Arusha kupitia ILO wanaendelea kutoa
mafunzo ya uanagenzi kwa vijana,pia Letshego Tanzania
kwa kujidhatiti kuwasaidia vijana kwa mikopo na
sapoti nafuu pia ushauri katika safari yao ya
kujikwamua kimaisha,wadau wengine ni wazara
ya Afya na kampeni yao ya NIPO TAYARI
wakihimiza usafi hasa wa maliwatoni kunawa mikono.
Kuelekea kuhitimisha Mh Mavunde alikubaliana
na mtazamo wa FURSA 2017 wa Anzia Sokoni
akithibitisha kua katika lolote lile lazima kujua soko linataka nini.
No comments