Header Ads

WALIOPIGWA 5-0, KOCHA ASEMA WACHEZAJI WALIKUWA WAKIIOGOPA SIMBA


Baada ya kushuhudia timu yake ikiambulia kipigo cha mabao 5-0 kutoka kwa Simba, Kocha wa timu ya Hard Rock, Muhibu Kanu amesema kuwa wachezaji wake walikuwa na hofu.

Kanu amesema kuwa mchezo huo umewasaidia kuona wapi ambapo kuna mapungufu katika kikosi chao ambapo watayafanyia kazi lakini akadai kuwa wachezaji wake walikuwa na hofu kwa kuwa waliona wancheza na timu kubwa.

Akizungumza baada ya mchezo huo, alidai kuwa ameona mapungufu na kwa kuwa ligi inatarajiwa kuanza hivi karibuni, basi Simba kilikuwa kipimo kizuri kwa wachezaji wake na benchi lao la ufundi limeshaona upungufu ulipo.

No comments

Powered by Blogger.