KATIBU MKUU WA CHADEMA AJISALIMISHA POLISI
Katibu Mkuu wa Chadema,
Dk Vincent Mashinji ameamua
kwenda kuripoti Makao Makuu
ya Jeshi la Polisi jijini Dar
Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu
na Mkuu wa Idara ya Habari
na Mawasiliano ya Chadema,
Tumaini Makene imesema
Dk Mashinji ameambatana
na wasaidizi wake kutoka
makao makuu ya chama hicho.
“Katibu mkuu amewasili Makao
Makuu ya Jeshi la Polisi,
jijini Dar es Salaam,
kuitikia wito wa Polisi
uliotolewa na Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Dodoma,
Gilles Muroto, kuwa anatakiwa
kufika Ofisi ya Mkurugenzi
wa Upelelezi wa Makosa
ya Jinai (DCI)” amesema.
Awali, leo Jumatatu Dk Mashinji
alisema hawezi kwenda kuripoti
kwa kuwa hakuambiwa siku
maalumu ya kwenda.
Kamanda Muroto amemtaka
Dk Mashinji afike ofisi ya Upelelezi
wa Makosa ya Jinai mkoani
Dodoma au ofisi kama hiyo
iliyopo Kituo Kikuu cha Polisi
Kanda Maalumu ya Dar es Salaam
ili kutoa ushirikiano kwa jeshi
hilo kuhusu tukio la kushambuliwa
kwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.
“Nina taarifa za kuitwa Polisi,
lakini haziko ‘specific’.
Ni wakati wowote naweza
kwenda? na hawajasema
nikaripoti wapi. Kwa hiyo,
wakinihitaji watakuja kuniambia,
” alisema Dk Mashinji leo asubuhi.
Lissu alipigwa risasi na watu
wasiojulikana Septemba 7
mchana alipokuwa akielekea
nyumbani kwake Area D mjini Dodoma.
Kwa sasa Lissu anaendelea
na matibabu katika Hospitali
ya Aga Khan jijini Nairobi, Kenya.
No comments