MUZIKI WA KAMUSOKO NA TSHISHIMBI KAMA KAWAIDA JANGWANI
Baada ya kushindwa kumaliza mchezo
dhidi ya Njombe Mji, kiungo wa Yanga,
Thaban Kamusoko amerejea kwenye
mazoezi baada ya kupata ruhusa ya daktari.
Kamusoko alianza mchezo huo vizuri
Kamusoko alianza mchezo huo vizuri
kwenye Uwanja wa Sabasaba ambapo
timu yake ilipata ushindi wa bao 1-0,
lakini alishindwa kumaliza dakika 90
ambapo alitoka kipindi cha pili na
nafasi yake kuchukuliwa na Rafael Daudi.
Haikujulikana kwa haraka juu ya
Haikujulikana kwa haraka juu ya
kilichosababisha akashindwa
kuendelea kucheza licha ya kutoka
uwanjani akitembea mwenyewe
bila msaada wa mtu yeyote.
Ofisa Habari wa Yanga, Dismas Ten
Ofisa Habari wa Yanga, Dismas Ten
amesema kuwa Kamusoko alipata
majeraha madogo lakini alirejea
uwanjani leo Jumatatu na kuendelea
na mazoezi kama kawaida baada ya
kuruhusiwa na daktari wa timu aliye
mfanyia uchunguzi.
No comments