MAASKOFU WATOA TAMKO KUHUSU LISSU KUSHAMBULIWA
(TEC), limelaani shambulizi la hivi
karibuni lililotekelezwa na watu
wasiojulikana dhidi ya Mbunge
wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.
Mbunge huyo aliyejeruhiwa Septemba 7
kwa kupigwa risasi tano mjini Dodoma,
hivi sasa anaendelea na matibabu
katika Hospitali ya Aga Khan,
jijini Nairobi nchini Kenya.
Baraza pia limeungana na Watanzania
kulaani kwa nguvu zote matendo yote
ya vurugu, mauaji na uvunjifu wa amani nchini.
Tamko la baraza hilo lililosainiwa na
Makamu wa Rais wa TEC, Askofu
Beatus Kinyaiya limetolewa baada
ya kikao cha kawaida cha baraza
kilichofanyika kwa siku mbili Septemba
9 na 10 jijini Dar es Salaam.
“Katika Taifa letu sasa tunashuhudia
matendo ya mauaji ya watu wasio
na hatia kama ilivyokuwa kule Mkuranga,
Rufiji na Kibiti, utekwaji wa watu na kuteswa,
utekaji wa watoto, ulipuaji wa ofisi za watu na
hivi karibuni shambulio la mbunge Lissu,”
limesema baraza katika tamko hilo.
Imeelezwa vurugu na mashambulizi ya
aina yoyote ile yanalifedhehesha Taifa
kwa kuwa matendo hayo ni dhambi,
uhalifu na si utamaduni wa Mtanzania,
hivyo vyombo vinavyohusika havina budi
kuyakomesha mara moja.
No comments