SHAIRI: MWANAFUNZI WA CHUO ALIYEDISCO KISA UTAMU WA PENZI LA PROFESA
TABORA TANZANIA
Hadithi hadithi njoo, eti
utamu kolea,
Staff ni Kariakoo, kama shuleni ni Daa,
Porofesa shikamoo, penzi
lako lanikolea,
Tamu penzi la profesa, limefanya nimedisco.
Stori ilianzia lekcha, tangia
mwaka wa kwanza,
Nilipomuita ticha, kumbe
ajua kufunza,
Macho nikayapikicha, kidole
kikawa funza,
Tamu penzi la profesa, limefanya nimedisco.
Quiz aloitoa, mimi simo darasani,
Hofu ikaniingia, nikaenda
ofisini,
Goti nikampigia, pate
maksi kilaini,
Tamu poenzi la profesa, limefanya nimedisco.
Mwenyewe kanifukuza, hataki
hata niona,
Machozi nikajiliza, mwenyewe
huku kanuna,
Mafua kuyapuliza, huruma
pate iona,
Tamu penzi la profesa,limefanya nimedisco.
Mara katoa kauli, nenda uje baadaye,
Nikahisi ni kivuli, mwanga uje ung'aye,
Nikasema afadhali, kumbe
ni kajiandaye,
Tamu penzi la profesa, limefanya nimedisco.
Muda nao kawadia, nikaenda
ofisini,
Miwani akaivua, kalamu
kaweka chini,
Nataka kusaidia, kwa pozi
na umakini,
Tamu penzi la profesa, limefanya nimedisco.
Kama unataka maksi, mimi
nataka mapenzi,
Wala siwe wasiwasi, ntakulinda
ntakuenzi,
Pesa tele kwa nafasi, nitakupa
nalo Benzi,
Tamu penzi la profesa, limefanya nimedisco.
Moyo kajawa tamaa, kawa
sitaki nataka,
Akili ilikataa, huku moyo
ukataka,
Neno zito nikatoa, profesa
akaniteka,
Tamu penzi la profesa, limefanya nimedisco.
Na vile sinaga bumu, kwangu
ikawa neema,
Vile maisha magumu, kwa
tabu ninavyosoma,
Nikampenda mwalimu, penzini
zama mazima,
Tamu penzi la profesa, limefanya nimedisco.
Tukaanza kwenda klabu, wikendi
hasa usiku,
Tukaanza gonga ulabu, baga piza chipsi kuku,
Kwangu ni mwisho wa tabu,
sasa mimi si kapuku,
Tamu penzi la profesa, nimefanya nimedisco.
Nikasahau na shule, kutwa
nipo na profesa,
Leo huku kesho kule, tunakula
tu anasa,
Nikampa penzi tele, muziki
kama darasa,
Tamu penzi la profesa, limefanya nimedisco.
Penzi likaninogea, nikapoteza
ramani,
Semista ikapotea, ikafika
mitihani,
Shule kaingia doa, nikafeli
siamini,
Tamu penzi la profesa, nimefanya nimedisco.
Sasa muda wa aris, moyoni
ni tetemeko,
Nikawa na wasiwasi, moyoni
mfadhaiko,
Nilihisi mkosi, matokeo
nimedisco,
Tamu penzi la profesa, limefanya nimedisco.
Narudi home najuta, kutwa
kulia machozi,
Nichotaka nimepata, narudi
kwao wazazi,
Nakumbuka ninajuta, hili
funzo la kizazi,
Tamu penzi la profesa, limefanya nimedisco.
Na Shablil President
Wa Nyamwezi Kingdom
2017 Kamilishamalengo
0718615269/0763902318
No comments