WAZIRI MKUU MSTAAFU AMJULIA HALI TUNDU LISSU
Waziri Mkuu wa zamani, Edward
Lowassa yupo Nairobi nchini
Kenya kumjulia hali Mbunge
wa Singida Mashariki, Tundu
Lissu aliyelazwa katika Hospitali
ya Aga Khan, baada ya kushambuliwa
kwa risasi na watu wasiojulikana.
Lissu ambaye pia ni mwanasheria
wa Chadema alijeruhiwa kwa
risasi tano Alhamisi Septemba 7
akiwa ndani ya gari nyumbani
kwake Area D mjini Dodoma
akitokea bungeni.
Katika akaunti yake ya Twitter,
Lowassa ame-tweet akisema,
“Earlier today i paid a visit at
Nairobi Hospital to see our
MP, President of TLS and
dear friend @tundulissutz
He is recovering well.
It is Sad times for Tanzania.
Let us all keep praying.”
Kwa tafsiri isiyo rasmi amesema
“Mapema leo nilitembelea
Hospitali ya Nairobi
kumwona mbunge,
Rais wa Chama cha Wanasheria
wa Tanganyika (TLS) na
rafiki kipenzi Tundu Lissu.
Anaendelea vizuri. Ni kipindi
cha masikitiko kwa Tanzania.
Kwa pamoja tuendelee kuomba.”
Katika tweet hiyo, Lowassa
ambaye ni Mjumbe wa Kamati
Kuu ya Chadema, ameweka
picha akiwa pamoja na Alicia
ambaye ni mke wa Lissu;
Mwenyekiti wa Chadema,
Freeman Mbowe na dereva
wa Lissu Simon Mohamed Bakari.
No comments