MATOKEO YA MICHEZO YA UEFA ILIYOPIGWA JANA. ,MESSI AMEVUNJA REKODI HII
ya michuano ya UEFA Champions League
msimu wa 2017/2018 imechezwa usiku wa
Jumanne ya September 12 2017 barani Ulaya,
FC Barcelona wamecheza mchezo wao wa
kwanza dhidi ya Juventus ya Italia katika
uwanja wa Nou Camp.
Barcelona wakiwa katika uwanja wao wa
Nou Camp wameendeleza rekodi yao kwa
kucheza mchezo wao wa 23 wa UEFA
Champions League hatua ya Makundi
katika uwanja wake wa nyumbani pasipo
kupoteza wakiwa wametoa sare game mbili pekee.
Lionel Messi leo kwa mara ya kwanza amefanikiwa kumfunga golikipa wa Juventus Gianluigi Buffon akicheza dhidi yake mara nne baada ya kufanikiwa kumfunga magoli mawili katika ushindi wa magoli 3-0, magoli akifunga dakika ya 45 na 69 baada ya Ivan Rakitic kuifungia Barcelona goli la pili dakika ya 56.
No comments