KIPA ALIYEDAKA SIMBA DAY AMEFARIKI DUNIA
Ulimwengu wa soka leo umepata pigo jingine
baada ya kumpoteza mchezaji wa kimataifa wa
Ivory Coast aliyokuwa anaichezea Beijing
Enterprises Cheick Tiote, leo zimeripotiwa
habari za kufariki kwa golikipa wa club ya
Rayon Sports ya Rwanda Evariste Mutuyumana.
Golikipa wa Rayon Sports Evariste Mutuyumana
amefariki dunia baada ya kupata tatizo la kushindwa
kupumua vizuri, kama utakumbuka vizuri Evariste
Mutuyumana ni miongoni mwa wachezaji wa Rayon
waliyokuja Tanzania kucheza na Simba katika
mchezo wa Simba Day.
Evariste Mutuyumana ndio golikipa wa Rayon
Sports aliyedaka katika mchezo wa Simba Day
August 8 2017 uwanja wa Taifa Dar Es Salaam
na Simba kufanikiwa kupata ushindi wa goli 1-0
lililofungwa na kiungo wao Mohamed Ibrahim
dakika ya 16.
No comments