BUNGE LAMUAHIDI USHIRIKIANO JAJI MKUU MPYA
Spika wa Bunge la Tanzania,
Job Ndugai amefunguka na kudai
atahakikisha yeye na wabunge wanampa
ushirikiano Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Hamis
Juma aliyeapishwa leo baada ya kuteuliwa
siku ya jana Septemba 10 mwaka huu.
Ndugai ametoa kauli hiyo wakati
alipokuwa anatoa salamu za
wabunge katika ghafla hiyo ya
uapisho iliyofanyika katika
viwanja vya Ikulu Jijini
Dar es Salaam na kuhudhuriwa
na viongozi mbalimbali wa
kitaifa bila ya kumsahau
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
"Sisi kama bunge tunawahakikishia
ushirikiano mkubwa sana kwa
kuhakikisha kazi za Mahakama
zinaendelea kama zilivyo kikatiba
na tutaheshimu sana. Yale
maneno na makombora moja
moja ya bungeni ni vitu vya
kawaida, ndiyo utamadun
i wa bunge",amesema Ndugai.
Aidha, Ndugai amesema
Mahakama inamchango
mkubwa kwa wananchi
pamoja na taifa kwa
ujumla kwa kuwa hicho
ndicho chombo
pekee kinachoweza
kumtetea mnyonge
kuweza kupata haki
yake kutoka kwa waporaji.
"Kuwepo kwa Mahakama
ndiyo usalama wetu,
amani, kheri na matumaini
ya mnyonge katika sheria
na maamuzi ya Mahakama.
Kwa hiyo tunakutakia kila
la kheri katika kazi yako,
tunakuombea kwa
Mwenyezi Mungu
na tutakusaidia na
kuomba msaada wako",amesisitiza Ndugai.
Kwa upande mwingine,
Jaji Mkuu Prof. Ibrahim
Hamis Juma ameahidi
kufanya kazi katika
maadili ya kisheria pamoja
na kurudisha imani ya
wananchi kuhusiana na
kupata misaada ya
kisheria inayotolewa
katika Mahakama mbalimbali
ndani ya Tanzania
No comments