Header Ads

UTANI WA MANARA UMEHAMIA KWA WENGER

Moja kati ya stori zinazotrend kwa sasa ni kuhusiana na klabu ya Arsenal kutofanya vizuri chini ya kocha wao wa muda mrefu Arsene Wenger, kocha huyo amekuwa akisifika kwa ubahili na kupenda kusajili wachezaji kwa dau dogo.
Afisa habari wa Simba Haji Manara ni mmoja kati ya watu wanaopenda soka la England lakini pia ni moja kati ya watu wanaopenda kuwatania mashabiki wa Arsenal ambao timu yao haifanyi vizuri kwa sasa.
Haji Manara kupitia ukurasa wake wa instagram ameandika kwa utani kuwa amepokea simu kuwa Arsenalwameomba kumsajili beki wao mganda Juuko Murshid lakini hawamuuzi kwa sasa hadi kocha Wengeraondoke.
“Nimepokea CM ya Babu Wenger anaulizia ofa yetu kuhusu Juuko Murshid,,nimemjibu hatumuuzi kwao mpaka yy aondoke Arsenal!! @mwanafa#JuukoMurshid

No comments

Powered by Blogger.