MBAO YAENDELEA KUPOKEA VICHAPO MECHI ZA KUJIPIMA NGUVU.
Klabu
ya Mbao bado haijakaa vizuri baada ya kuchezea vichapo viwili mfululizo
kwenye mechi za kujipima nguvu iliyocheza hivi karibuni.
Timu hiyo yenye maskani yake Sabasaba wilayani Ilemela jijini
Mwanza, imeweka kambi yake katika Chuo cha Ualimu Butimba mkoani hapa ikijiandaa na Ligi Kuu Bara.
Mbao
ilianza kuwajaribu wachezaji wake Jumamosi ya wiki iliyopita kwa
kucheza na Mwadui na kumaliza mtanange huo kwa kisago cha mabao 3-1.
Kama
haitoshi,wakata Mbao hao wa jijini hapa walirudi uwanjani tena Jumapili
kuwakabili Pamba FC inayojiandaa na Ligi Daraja la kwanza na kuambulia
kichapo cha mabao 2-0.
Kutokana na
hali hiyo, Kocha wa Makipa wa Mbao FC, Soud Slim alisema matokeo hayo
hayawezi kuwapa presha au kuwakatisha tamaa na kwamba timu yao ni nzuri.
Alisema
kuwa wao kama benchi la ufundi kwa sasa wanahitaji kutengeneza
kombinesheni, hivyo suala la matokeo kwenye mechi za kirafiki si
kipaumbele.
“Kumbuka hapa tunajaribu
mitambo tu, hatuangalii wala kutafuta matokeo, tunataka kutengeneza
kombinesheni ya wachezaji na kuona wapi turekebishe,” alisema Slim.
Aliwataka
wadau na mashabiki wa timu hiyo na Mkoa kwa ujumla kuwa na subra na
kusema kuwa Mbao itakuwa timu bora na yenye ushindani tofauti na msimu
uliopita.
No comments