Header Ads

NYUMA YA PAZIA: MO MASHINE…

Image result for mohamed ibrahim mo simba 2017



Soka ni mchezo unaochezwa hadharani yaani kila mtu anaushuhudia. Lakini katika mchezo huu kuna mambo mengi hujitokeza na ndiyo mambo haya ambayo hufanywa na wachezaji kwa kiasi kikubwa huwafanya wachezaji hao kujulikana na kuwa na majina makubwa.

Lakini kama ilivyo kipengele hiki cha nyuma ya pazia hiki huangazia zaidi pale ambapo upeo wa macho ya mwanadamu haufiki kirahisi. Na leo umekuja kumuangazia kiungo mshambuliaji wa Simba Mohamed Ibrahim.

Mchezaji huyu huwa hasemwi sana na vyombo vya habari hata watu wenyewe huwa hawamsemi sana. Labda jambo hili ndilo humfanya hata kocha kutowaza kumuanzisha katika mechi muhimu kinyume chake humuacha nje katika benchi asubiri timu izidiwe ndiyo aingie kama mkombozi.

Kila shetani na mbuyu wake hivyo huenda mbuyu wa Mohamed Ibrahim Cabaye ukipenda muite MO ni kuanzia benchi. Moja kati ya wachezaji muhimu kabisa katika klabu ya Simba ni MO ndiyo maana hata kipindi Ibrahim Ajib anahama timu basi mashabiki na wapenzi wa Simba walijinasibu kwa kusema “Ajib yeye aende tu, tunaye MO”.

Kijana huyu aliyesajiliwa kutokea Mtibwa Sukari ya Manungu Tuliani Morogoro, anavalia jezi nambari 4, iliyokuwa ikavaliwa na Hassan Kessy aliyehamia Yanga huku yeye akitua hapo na kuichukua mwanzoni mwa msimu uliopita.
Tangu ametua Simba amekuwa katika kiwango cha hali ya juu kitu kinachomfanya sasa kuonekana kama mkombozi wa timu pale inapozidiwa utasikie “muingize MO ndani”. Kauli hizi si za utani bali ni uhalisia kwa kijana huyu ambaye kila akicheza mathalani kwa kutokea benchi amekuwa akifanya makubwa na kugeuka lulu ya Msimbazi.
Labda nukukumbushe michezo kadhaa ambayo amekuwa akicheza mara nyingi amekuwa akienda kupindua matokea na muda mwingine akifunga yeye mwenyewe. Kuna wakati aliumia na pengo lake likaonekana.

Mchezo wa kwanza ninaotaka tuuzungumzie ni ule wa nusu fainali kati ya Simba na Azam uliochezwa uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam na kumalizika kwa Simba kushinda kwa goli 1 – 0. Goli pekee katika mchezo huo lilifungwa na Mohamed Ibrahim MO CABAYE dakika chache kabla hajalimwa kadi ya njano ya pili na mwamuzi kuamua kumtoa nje kwa kadi nyekundu. Licha ya kutolewa kwa kadi nyekundu lakini goli lake lilidumu na kuifanya Simba kutinga fainali na hatimaye kuibuka bingwa wa kombe la FA, hivyo kukata kiu yao ya vikombe lakini pia kuweza kukata tiketi ya kushiriki michuano ya kimataifa ya kombe la Shirikisho barani Afrika.

Image result for mohamed ibrahim mo simba 2017
Tarehe 8 Agosti mwaka huu Simba ilishuka dimbani kumenyana na klabu ya soka ya Rayon Sports ya Rwanda siku ya kilele cha maadhimisho ya Simba Day. Mchezo huo ambao hutumika kutambulisha wachezaji mathalani wapya uliochezwa uwanja wa taifa jijini Dar es salaam, ulimalizika kwa Simba kushinda ushindi mwembamba wa goli 1 – 0. Goli pekee likifungwa na Mohamed Ibrahim MO CABAYE. Kutoakana na usajili uliofanya na klabu hiyo mwaka huu ingekuwa aibu kubwa sana kwenda suluhu na bingwa hao wa Rwanda, si kwa sababu Rayon hawajui mpira la hasha, bali ni kutokana na tambo na mbwebwe za mashabiki wa Simba. Na goli hilo la MO lilitosha kabisa kufuta aibu hiyo badala yake kuamsha ndelemo vifijo na shamrashamra katika mitaa ya Msimbazi.

Jumatano Agosti 23, 2017, MO anaingia katika rekodi kubwa ya soka la Tanzania kwa kuiwezesha klabu yake kuchukua taji la ngao ya jamii. Alipiga penalti ya mwisho kwa ufundi na ustadi wake na kuifanya Simba kuwa mabingwa. Licha ya kwamba alichelewa kuingia lakini kiwango chake kilikuwa kizuri cha halio ya juu.

Image result for mohamed ibrahim mo simba 2017

Jambo zuri ni kwamba MO ameumbika kisoka amestaarabika kiuchezaji hivyo kuwa miongoni mwa lulu za mpira wetu. Nmamuona MO katika moja ya vilabu vikubwa Ulaya tena katika ligi kubwa na Mwenyezi Mungu amuwezeshe kutimiza jamabo hili kwani anatashili kabisa bila ya kumung’unya maneno au kupepesa macho macho.

Kila la kheri MO.


Weka maoni yalo hapa.

No comments

Powered by Blogger.