Header Ads

NYUMA YA PAZIA: WACHEZAJI BORA 11 WANAOUNDA KIKOSI CHA KWANZA NGAO YA JAMII.

Image result for simba na yanga

Shaaban Maulidi #MaulidiTV

Mchezo wa kandanda ndiyo mchezo unaopendwa na watu wengi zaidi duniani na hapa Tanzania bila shaka mchezo huu ndiyo unaopendwa zaidi. Lakini mapenzi yanazidiana na hii haimaanishi tu kila timu inayosakata kabumbu basi ndiyo ipendwe sawa na nyingine.

Kwa hapa Tanzania unapozungumzia soka basi huwezi kuacha kuzitaja klabu za Simba na Yanga ambazo zimebeba jina na uzito wa kandanda la Tanzania. Siku ya Jumatano Agosti 23 2017, timu hizi zilikutana katika dimba la Taifa kupepetana ili kuweza kulichukua taji la Ngao Ya Jamii, ambalo  muhimu katika kuweka rekodi zao vizuri.

Hapa nimekuwekea idadi ya wachezaji 11 wanaounda kikosi cha kwanza katika pambano hilo, kulingana na kiwango cha uchezaji waliokionesha lakini yote kwa yote ni kwa mtazamo na maono ya mwandishi wa Makala hii.

1.      AISH MANULA.

Image result for manula aishi

Kwanza huyu ndiye Mlinda mlango nambari moja kwa Timu ya Taifa ya Tanzania kwa sasa. Amesajiliwa na Simba akitokea Azam ambako amelelewa na kucheza kwa muda mrefu. Ni kijana mdogo ambaye ni hazina kubwa ya taifa mathalani katika ulimwengu wa soka. Katika mchezo wa ngao ya jamii ameonesha na kudhihirisha ni kwa nini mwalimu wa kikosi cha timu ya taifa kumwamini na kumfanya mlinda mlngo nambari moja, pia maeonesha thamani ya usajili wake Simba. Ameokoa michomo ya hapa na pale japo hakupata kashikashi za kutoka. Ameoangua penalti ya kwanza na kuisadia klabu yake kuibuka mshindi.

2.      ALLY SHOMARI

Image result for ally shomari

Kijana aliyesajiliwa akitokea Manungu Tuliani mkoani Morogoro alipokuwa akikipiga na wakata miwa wa Mtibwa Sukari.  Hakuna aliyetarajia kuwa ataanza lakini huenda kutokuwepo kwa Shomari Kapombe kulimpa nafasi ya kucheza. Ameonesha kiwango kizuri cha kukaba wachezaji wazuri wa Yanga lakini aliweza kupandisha mashambulizi. Anaonekana ni mwenye kutumia akili na nguvu pia.

3.      GADIEL MICHAEL.

Image result for gadiel michael yanga




Atakumbukwa sana na wapenzi na mashabiki wa timu ya Azam, lakini kwa sasa ni mchezaji wa Yanga. Kijana huyu ni mchezaji mwenye kiwango cha hali ya juu lakini vilevile ana kiapji kikubwa. Amecheza vizuri katika nafasi yake na kuwafanya kina Okwi na KIchuya kushindwa kuwika lakini pia uwezo wake wa kupandisha mashambulizi kunamfa kuwa bora zaidi.

4.      SALUM MBONDE

Image result for salum mbonde simba 2017

Ni mchezaji mwingine kutokea Mtibwa Sikari aliyesajiliwa Simba msimu huu. Ana akili sana anapokuwa uwanjani ana usafi wa matendo, utulivu wake pia humpamba zaidi na kumfanya aoanekane bora kuliko wenzake uwanjani. Kwa siku ya jana ameonesha kiwango kizuri hivyo natshili kuwemo katika kikozi cha kwanza.

5.      METHOD MWANJALE.

Image result for mwanjali wa simba

Wenyewe wanamwita baba mwenye nyumba, uzoefu wake, akili, nguvu na ukomavu wake ndivyo vimefanya akwepe panga la kutemwa licha majeruhi yaliyokuwa yakimsibu. Mwanjale kwa jana ameonesha kiwango kikubwa sana na anastahili kuwemo pia katika kiosi hiki.

6.      PAPPY KABAMBA TSHISHIMBI.

Image result for tshishimbi  yanga 2017

Sio mwenyeji sana lakini jina lake kwa sasa ni maarufu sana, amefanya mazoezi na Yanga kwa muda mchache lakini kwa kiwango alichokionesha jana si haba. Ana jicho lakuuona mpira, anakaba, anatoa pasi nzuri zenye macho na alifanikiwa kabisa kuituliza timu ya Yanga. Huyu ndiye anastahili kuitwa Nyota wa Mchezo.

7.      SHIZA KICHUYA.

Image result for kichuya

Hapa hakuna mwenye swali la kwa nini bwana mdogo huyu mwenye maajabu ya kipekee katika soka hasa la Tanzania. Kichuya atakumbukwa milele kwa goli la kona ya moja kwa moja lakini lile lililomfanya achukue tuzo ya goli bora la Msimu wa 2016/2017 siku ya jana pia alikuwa katika ubora wake.

8.      MZAMIRU YASSIN

Image result for mzamiru yassin

Huyu jamaa uwanjani huwa kama hayupo vile, lakini inapokuja suala la tathmini basi inakuwa ni vigumu sana kumuacha. Amecheza vizuri sana na anafaa kuwa katika kikosi hiki kwani uwezo wake kwa siku ya jana ulikuwa ni wa kiasi kikubwa mno.

9.      IBRAHIM AJIB

Image result for ibrahim ajib yanga

Wengi watauliza kwa nini yupo katika nafasi hii lakini ukweli ni kwamba Ajib ndye mshambuliaji aliyeonesha kiwango kikubwa katika pambano la jana hivyo anatashili kuwemo na kuwa katika nafasi hii. Haji Sunday Manara aliwahi kusema ya kuwa “ukiwaacha Diamond na Alikiba binadamu pekee anayetoa burudani ya hali ya juu ni kijana huyu”. Kuhama kwake Simba hakumfanyi kuwa ameshuka kiwango bali ubora wa Ajib unafahamika hadi kwa yule mtoto mdogo aliyechora shati lake namba na jina la Ajib.

10.  EMMANUL OKWI

Image result for emmanuel okwi 2027

Unaweza kumuita mfalme wa Simba kama mabavyo wenyewe wanamuita. Amekuwa kipenzi cha wapenda soka kwa aina ya uchezaji wake na msaada wake katika timu. Siku ya jana aliweza kucheza vizuri sana kiasi cha kutosha kuonekana katika orodha hii.

11.  HARUNA NIYONZIMA.

Image result for haruna niyonzima asaini simba

Huyu ndiye Fabregas wa Afrika Mashariki, jina hili hakupewa kwa sababu ya kufanana kwa sura na yule kiungo wa Chelsea Cesc Fabregas la hasha, bali ni kwa aina ya uchezaji wake. Pasi zaake murua, chenga na kujituma mdiko kumemfanya aweze kuingia katika oroidha hii.

Tupe maoni yako hapa.

No comments

Powered by Blogger.