Header Ads

NYUMA YA PAZIA: LICHA YA SIMBA KUCHUKUA UBINGWA LAKINI LAZIMA WAZINGATIE HAYA.

Image result for SIMBA MABINGWA NGAO YA JAMII 2017














Siku ya jana ni muhimu pengine pengine kuliko siku za hivi karibuni kwa klabu ya Simba. Umuhimu wake hapa si wa kuchukua ubngwa wa Ngao ya Jamii, bali nikuchukua kikombe mbele ya mahasimu wao wa jadi yaani Yanga tena kwa kuwafunga.

Macho na masikio ya watanzania wengi yalielekezwa pale wilayani Temeke katika dimba la taifa lililokaribiana kabisa na Chuo Kikuu Kishiriki Cha Cha Elimu Dar es salaam (DUCE), ambapo watani wa jadi Simba na Yanga walikuwa wakipepetana vikali.

Kabla ya kuanza kwa pambano hilo kulikuwa na tambo za hapa na pale wakati Haji Sunday Manara akiwaandaa mashabaiki na wapenzi wa Klabu hiyo kuwa Yanga lazima afe si chini ya goli 5, Salum Mkemi yeye akizungumza dakika chache kabla ya pambano kuanza aliwaonya mahasimu wao Simba kuwa matokeo waliokuja nayo mikononi wayaache wsubiri dakika 90.

Kwa kuwa siku hazigandi basi hata muda nao hausimami, hatimaye lile pambano lililokuwa likisubiriwa kwa hamu likaanza mnamo majira ya saa 11: 00 za jioni. Simba inayonolewa na Joseph Omog iliwaanzisha Aishi Manula, Ally Shomari, Erasto Nyoni, Salum Mbonde, Method Mwanjale, Shiza Kichuya, Mzamiru Yassin, Laudit Mavugo, Emmanuel Okwi na Haruna Niyonzima. Yanga waliwaanzisha Rostand Youthe, Juma Abdul, Gadiel Michael, Andrew Vicent, Kelvin Yondani, Pappy Tshishimbi, Emmanul Martine, Thabani Kamusoko, Donald Ngoma, Ibrahim Ajib na Raphael Daud.

Mchezo ulikuwa mzuri kiasi chake lakini haukuwa na ladha ambayo tuliambiwa na kuitegemea hivhyo kuufanya uwe wa kawaida kama alivyotabiri Massau Bwire. Baada ya dakika 90 kukamilika kwa sare tasa ya bila kufungana ndipo ilipomlazimu mwamuzi Elly Sassy kulipeleka pambano hilo kuamuliwa kwa changamoto ya Mikwaju ya penalti huku Simba ikiibuka na ushindi wa penalti 5 – 4 za Yanga.

Simba wanastahili pongezi kwa hili lakini jambo la kuzingatia ni kwamba bado safu yao ya ushambuliaji inayoongozwa na Laudit Mavugo bado ni butu huku ikishindwa kuzifumani nyavu za timu pinzani. Ikumbukwe ya kuwa msimu uliomalizika Simba ilikosa taji la ligi kuu ambalo kwa miaka kadhaa imekuwa ikilisotea lakini wakalikosa kwa tofauti ya idadi ya magoli ya kufunga na kufungwa na kuwaacha Yanga wao waliokuwa na hazina ya kutosha ya magoli kulichukua kombe hilo mara tatu mfululizo.

Nilichokiona kwa Mavugo si mchezaji wa kubezwa hata kidogo tena naweza kuthubutu kusema ya kuwa huyu ndiye mshambuliaji bora kwa sasa, lakini jambo ambalo mwalimu Omog anatakiwa alizingatie ni namna ya kumtumia mchezaji huyu kwani amekuwa akikosa utulivu pia amekuwa akihama mara kwa mara kwenye nafasi yake hivyo kuwaacha mabeki wakiwa huru bila ya kash kash ya hapa na pale. Kama atapata utulivu huku Shiza Kichuya na Emmanuel Okwi na Niyonzima wakijua kumtumia basi ile rekodi aliyoiweka kwenye ligi ya kwao atakuja kuiweka na hapa Tanzania.
Suala la viungo kwa jana walipwaya muda mwingi na kumuacha Tshishimbi akiwa mmiliki halali wa dimba la katikati, huku Mwalimu Omog akionesha udhaifu wa kushindwa kumwingiza Jonas Mkude ambaye anaaminika kuwa ndiyo mwenye dimba lake pale katikati. Suala la mabeki wa simba kujiamini uda mwingi ni zuri lakini kuna muda lilitaka kuwagharimu na kama si umahiri wa mlinda mlango Aishi Manula basi huenda shughuli ingeisha mapema.


Simba imekuwa na bahati ya kupata mabeki wa pembeni wazuri na siku ya jana Ally Shimari na Erasto Nyoni walionesha kiwango cha juu kabisa. Hivyo ni wito wangu kwa benchi la ufundi kulifanyia kazi tatizo la umaliziaji hasa kwa Mavugo. Kama atatengenezwa vizuri basi msimu huu kiatu cha dhahabu itakuwa ni halali yake huku kila aina ya kombe likiishia mikononi mwa Simba.

Na Shaabani Maulidi #MaulidiTV

No comments

Powered by Blogger.