SUP SIO KILEMA
Sup kwangu si kilema, ni
matokeo ya kitaaluma,
Kama kusoma nilisoma, mitihani
nikajibu vema,
Moduli zote zilituama, imenitokea
haijaniuma,
Sup Sio Kilema, tunasapua
Tunasepa
Sup ipo UDOM, Mzumbe hadi
SAUT,
Sup ipo UDSM, Makumira
hadi NIT,
Sup ipo na MUM, hadi
Mtwara ya SAUT,
Sup Sio Kilema, tunasapua
Tunasepa
Sup ipo kwa walimu, madaktari
na mafamasia,
Sup ipo kwa mahakimu, hadi
wale mainjiania,
Wahasibu na Masikomu, wanasiasa
na wanasheria,
Sup Sio Kilema, tunasapua
Tunasepa.
Yawahenga nayakumbuka, leo
kwangu kesho kwako,
Wewe unayenicheka, kesho
ni zamu yako,
Usijione umekamilika, UE
sio mjomba wako,
Sup Sio Kilema, tunasapua
Tunasepa
Tuunde na makundi, kwa
pamoja tujadili,
Hata sisi hatupendi, Imetokea
kama ajali,
Tulihudhuria vipindi, Biology
na Kiswahili,
Sup Sio Kilema, tunasapua
Tunasepa
Wapo waajiriwa, walisup
wakasapua,
Wapo wahemishiwa, walisup
wakasapua,
Wanasup sije pagawa, Semista
ijayo tutatoboa,
Sup Sio Kilema, tunasapua
Tunasepa
Wala usije jificha, ukasingizia
eti spesho,
Huo uoga jaribu acha, ili
usisup tena kesho,
Iwe semina iwe lekcha, jitahidi
kuvuja jasho,
Sup Sio Kilema, tunasapua
Tunasepa
Si kilaza si kipanga, yote
amepanga Mungu ,
Tena Sup Sio ujinga, nisikilizie
Rafiki yangu,
Tena Sup wala si janga, nitapata
degree yangu,
Sup Sio Kilema, tunasapua
Tunasepa.
Na Shaaban Maulidi
0718526159/ 0763902318
No comments