AFRICAN LYON YAWAWEKEA NGUMU WACHEZAJI WAKE.
Timu ya African Lyon imewawekea pingamizi wachezaji wake 19, akiwemo kipa Youth Rostand aliyejiunga na Yanga.
Afisa
Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF), Alfred Lucas alisema Kamati
ya Katiba na Hadhi za Wachezaji itakutana kuanzia Alhamis hii kupitia
mapingamizi hayo ili kuweka kila kitu sawa kabla ya Ligi Kuu Bara
kuanza.
"African Lyon imeondokewa na wachezaji wengi
waliohamia klabu nyingine na imewawekea pingamizi wachezaji wake 19
wakidai ada za uhamisho kutoka klabu walizotimkia, ada ya maendeleo, na
ada ya kuvunja mkataba"
" Pia, Kagera Sugar imemuwekea
pingamizi Mbaraka Yusuph kwa madai bado ni mchezaji wao kwani ana
mkataba na klabu hiyo, hivyo mapingamizi yote yatapitiwa na Kamati ya
katiba na Hadhi za wachezaji ambayo inaweza kukutana kuanzia Alhamis,"
alisema Lucas.
Alfred aliwataja wachezaji hao wa
African Lyon ambao wamewekewa pingamizi kuwa ni Rostand(Yanga), Saleh
Malande (Majimaji), Hamad Manzi, Mussa Nampaka, Lambele Jerome(Lipuli),
Hamad Waziri, Baraka Majogoo(Ndanda), Omary Salum, Fred Lewis (Coastal
Union), Abdallah Mguhi, Omary Abdallah, Venance Ludovic (Kagera Sugar).
Pia,
alisema Azam imewekewa mapingamizi mawili dhidi ya Kagera Sugar
wanaopinga kusajiliwa kwa mshambuliaji wao Mbaraka Yusuph na dhidi ya
Majimaji wanaopinga kusajiliwa kwa mchezaji wao Iddi Kipangulile.
No comments