SHAIRI: USITOE MIMBA
Shukuru wako muumba, vizuri
ame kuumba
Usichana kakuremba, amekupa
na mchumba
Kakunyima Na Ugumba, waweza
kubeba Mimba
Dada Usitoe Mimba, mtunze
Atakutunza
Kakupa na Sura nzuri,kakupa
na jina zuri
Kakupa na umbo zuri, kakupa
na afya nzuri
Kakupa na dini nzuri, kakupa
na hali nzuri
Dada Usitoe Mimba, mtunze
Atakutunza
Siku ulipo balehe, kwako
ikawa sherehe
Kukua jua starehe, kuchi
Kuchi Na Hotehe
Wala hukusamehe, ukadharau
mashehe
Dada Usitoe Mimba, mtunze
Atakutunza
Kama Hukutaka ndoa, ni
kwa nini ulivua
Penzi ukampatia, kwa raha
nazo hisia
Tena Utamu kolea, hadi
mimba kaingia
Dada Usitoe Mimba, mtunze
Atakutunza
Mama alikukataza, hiyo
michezo kucheza
Kisha akakakufunza, jinsi
ya kujitunza
Kiburi kimekuponza, kidoleni
sasa funza
Dada Usitoe Mimba, mtunze
Atakutunza
Ukawajua shababy, mara
Mume mara Hubby
Mara Sweet mara baby, mara
Sam mara shebby
Mara Chande mara Phabby,
ukahisi wewe Rubby
Dada Usitoe Mimba, mtunze
Atakutunza
Ukajifanya wajua, mapenzi
ukayavaa
Mahaba ukayatoa, Guest
mpaka Baa
Ukawa kiruka njia, leo
tumbo mekujaa
Dada Usitoe Mimba, mtunze
Atakutunza
Mimba yako ni jawabu, wala
sione aibu
Tena Mimba si ajabu, kutoa
siyo kutubu
Itunze yako thawabu, wala
sione adhabu
Dada Usitoe Mimba, mtunze
Atakutunza
Wala sije tapatapa, kutoa
kisha kutupa
Riziki Mungu kukupa, itunze
mithili chupa
Mungu atakuchapa, na
motoni kukutupa
Dada Usitoe Mimba, mtunze
Atakutunza
Ukitoa umeua, dhambi
zaidi zinaa
Mlee atakulea, mwanaume
kikataa
Wewe sikate tamaa, mimba
sije kuitoa
Dada Sitoe Mimba, mtunze
Atakutunza
No comments