SHAIRI KUHUSU WATOTO WA LUCKY VICENT: MEI SITA YA MAJONZI
Nawasha yangu kurunzi, nianze
andika utenzi,
Moyoni nina majonzi,
mwili wajawa na ganzi,
Ghafla nashusha pumzi,
kumshukuru Mwenyezi,
Ni
msiba wa taifa, mei sita ya majonzi.
Ghafla simu nafungua, WhatsApp naingia,
Taarifa zaenea, picha za
kusisimua,
Ajali imetokea,huko mlima
Rhotia,
Huu
msiba wa taifa, mei sita ya majonzi.
Gari limetumbukia, wanafunzi
limeua,
Thelathini na kadhaa, na
walimu wao pia,
Dereva hajabakia, tanzia
kote tanzia,
Huu
msiba wa taifa, mei sita ya majonzi.
Hao wanafunzi wetu, hao
ni watoto wetu,
Hao ni walimu wetu, hao
wote ndugu zetu,
Hao ni Kizazi chetu, poleni
wana Karatu,
Huu
msiba wa taifa, mei sita ya majonzi.
Pole kwa wao wazazi, walojawa
na majonzi,
Moyoni tuna simanzi, machoni
tuna machozi,
Hiyo kazi ya Mwenyezi, amefanya
kwa mapenzi,
Huu
msiba wa taifa, mei sita ya majonzi.
Kwa pamoja tunalia, tunalia
Tanzania,
Hii kwetu ni tanzia, huzuni
imetujaa,
Tuzidi kuwaombea, peponi
pakufikia,
Huu msiba wa taifa, mei sita ya
majonzi.
Tunapita hii dunia, hakuna
ato bakia,
Wao wametangulia, sisi
tutawafuatia,
Kikubwa kujiandaa, kwa
Mola kutubia,
Huu
msiba wa taifa, mei sita ya majonzi.
Walichanua maua, wamezima
kama taa,
Kifo mlango ni njia, sote
tutaupitia,
Kikubwa kujiandaa, ibada
zenye kufaa,
Huu
msiba wa taifa, mei sita ya majonzi.
Lucky
Vicent simanzi, kupoteza wanafunzi,
Tuliwapa na mapenzi, pamoja
bora malezi,
Kwarudisha hatuwezi, tumshukuru
Mwenyezi,
Huu
msiba wa taifa, mei sita ya majonzi.
Mwisho nizitoe pole, kwake
mkuu wa shule,
Wazazi watoto wale, watanzania
pia pole,
Njia yetu ile ile, hatutoishi
milele,
Huu
msiba wa taifa, mei sita ya majonzi.
Na Shaaban Maulidi
0718526159
No comments