Header Ads

OMOG, MAYANJA WAENDELEA "KUIDUNGA" SIMBA DOZI KWA AJILI YA YANGA


Kikosi cha Simba chini ya Kocha Joseph Omog na Msaidizi wake, Jackson Mayanja kimeendelea kula dozi hapa mjini Zanzibar.

Simba inajiandaa na mechi yake ya Ngao ya Jamii wikiendi ijayo dhidi ya Yanga kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Wachezaji wa Simba walionekana wako siriazi katika mazoezi ya Simba yanayofanyika kwenye Uwanja wa Amaan mjini hapa.

Hakuna aliyeosha utani hata kidogo, huku kila mmoja akijituma na kukimbia kwa kasi kubwa alipotakiwa kufanya hivyo.

Zaidi yaliyonekana ni mazoezi ya kutafuta unyumbulifu, umakini wa pasi na mengine kadhaa.




No comments

Powered by Blogger.