BREAKING NEWS : MBUNGE ESTER BULAYA APATWA NA HOMA KALI AKIWA MAHABUSU, AKIMBIZWA HOSPITALI
Mbunge wa Bunda mjini Mhe.Esther Bulaya, amekimbizwa hospitalini muda huu baada ya kuzidiwa akiwa mahabusu.
Daktari mfawidhi wa hospitali ya Wilaya Tarime amedhibitisha kumpokea Ester akiwa katika hali mbaya, kutokana na presha kushuka "below normal".
Ester amelazwa hospitalini hapo akiwa chini ya uangalizi maalumu wa madaktari.
Bulaya alikamatwa jana na jeshi la polisi akiwa katika hoteli ya Best Point Wilayani Tarime akidaiwa kujiandaa kutaka kufanya mkusanyiko kinyume cha sheria.
No comments