HABARI NJEMA KWA WASOMI WA LUGHA YA KISWAHILI KUTOKA KWA WASOMI WA KISWAHILI.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe
amelitaka Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) kuhakikisha inatengeza
kanzidata ya vijana wasomi wa lugha ya kiswahili wenye uwezo wa
kufundisha lugha hiyo duniani kote.
Dk Mwakyembe ameyasem hayo leo wakati alipotembelea katika ofisi za
Baraza hilo zilizopo Kijitonyama, Mnispaa ya Kinondoni jijini Dar es
Salaam ambapo amesema ni lazima kuwepo na kanzidata hiyo
itakayoorodhesha watalaamu wenye uwezo wa kufundisho lugha hiyo ikiwa
watatakiwa katika nchi yoyote dunian.
"Tunatakiwa tujiandae, nchi yoyote ikitaka mwalimu wa Kiswahili
tunapeleka, najumbuka tulishindwa kupeleka kwa Rais mmoja alitaka
mwalimu, hii ni aibu na ni kutojiandaa," amesema Waziri Mwakyembe.
Mtendaji Mkuu wa BAKITA, Selemani Sewangi amesema, baraza hilo lina
changamoto nyingivikiwamo uhaba wa fedha hali inayosababisha baraza hilo
kushindwa kufanya shughuli zake kwa ufanisi.
No comments