Header Ads

BREAKING NEWS; MAYANGA ABWAGA MANYANGA SIMBA



Wekundu wa Msimbazi SimbaSC wakielekea mchezo wao wa saba wa Ligi Kuu Tanzania bara msimu wa 2017/2018 dhidi ya Njombe Mji, zimeripotiwa taarifa za kuhuzunisha kuhusu kocha wao msaidizi Mganda Jackson Mayanja kujiuzulu.

Mayanja ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo ya ukocha msaidizi ndani ya Simba huku sababu zikitajwa kuwa ni zake binafsi na wala hakuna kingine ila AyoTV na millardayo.com zinaendelea kufatilia kwa kina kujua chanzo.

Kama utakuwa unakumbuka vizuri Jackson Mayanja alikuwa kocha msaidizi Simba toka akiwa na kocha Muingereza Dylan Kerr ambae baadae alifutwa kazi na nafasi yake Julai 1 2016 ikatangazwa kuchukuliwa na kocha Joseph Omog wa Cameroon.

Chanzo ni millardayo.com
 

No comments

Powered by Blogger.