MUGABE AGOMA KUNG'OKA MADARAKANI.
Rais wa miaka mingi
nchini Zimbabwe anaripotiwa kukataa kuandoka madarakana mara moja
licha ya kuongezeka wito wa kumtaka ajiuzulu.
Mugabe (93) aliwekwa
chini ya kuzuizi nyumbani wakati jeshi likichukua madaraka siku ya
Jumatano kufuatia mvutano kuhusu ni nani atamrithi.
Hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kuhusu mazungumzo yaliyofanywa Mugabe na ujumbe kutoka kanda hiyo pamoja na mapema.
Lakini taarifa zinasema kuwa amekataa kuondoka madarakani.
Kiongozi wa upinzani Morgan Tsvangirai amisema mapema kuwa kwa manufaa ya watu Mugabe,anastahili kujiuzulu mara moja.
Jeshi lilichukua hatua baada ya Rais Mugabe kumfuta
makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa, wiki iliyopiya, na kuashiria kuwa
alimpendelea mke wake Grace Mugabe, kuchukua uongozi wa chama cha ZANU-PF na kuwa rais.
Taarifa zinasema kuwa Mugabe ambaye alikuwa
madarakani tangu nchi hiyo ipate uhuru mwak 1980 anakataa kuondoka kwa
hiari kabla ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kuandaliwa mwaka ujao.
Baadhi
ya wadadisi wanasema kuwa Bw. Mugabe anaweza kujaribu kujihakikishia
usalama na familia yake kabla ya kuondoka madarakani.
Maafisa wa
Zanu PF mapema walikuwa wamesema kuwa Bw. Mugabe atasalia madarakani
hadi ufanyika mkutano mkuu wa Chama mwezi Disemba wakati Bw. Mnangagwa
atakiongoza chama na hatimaye kuwa rais.
Imepewa nguvu na BBC Swahili.
No comments