Header Ads

HATIMAYE MGOMO WA MADAKTARI WAKENYA UMESITISHWA RASMI.

Viongozi wa muungano wa wauguzi wakiongozwa na katibu mkuu wa muungano huo Seth Panyako

Wakenya sasa wamepata matumaini nmapya baada ya wauguzi wanaofanya kazi katika hospitali za umma kukubali kusitisha mgomo wao uliochukua takriban miezi mitano.
Katibu mkuu wa Muungano wa wauguzi {Knun} Seth Panyako aliwaambia wauguzi kurudi kazini mara moja.

''Hatimaye tumesitisha mgomo na tunawataka wanachama wetu kurudi kazini ifikiapo Ijumaa saa kumi na moja jioni'', alisema.
Mwenyekiti wa magavana nchini Kenya Josphat Nanok amesema kuwa makubaliano hayo na wauguzi yaliafikiwa baada ya majadiliano makali.

''Tumeafikia mwafaka na serikali wa marupurupu ya wauguzi pamoja na yale ya nguo za kazi za wauguzi mbali na marupuru ya kuwa hatarini kulipwa katika kipindi cha mwaka wa fedha cha 2018-2019'', alisema Nanok.
Kulingana na makubaliano ,wauguzi wataanza kupokea marupuru ya nguo za kazini za ksh.15,000 kuanzia mwaka wa kipindi cha fedha cha 2018-2019.

Marupurupu hayo yameongezeka kutoka 10,000 waliokuwa wakipata .
''Marupurupu hayo pia yataendelea kuongezwa kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo baada ya kipindi cha bajeti cha 2018-2019'', aliongezea Nanok. 

Vilevile wauguzi hao wataanza kupokea marupurupu ya kuwa hatarini ya kati ya ksh.20,000 na ksh.25,000 za Kenya kulingana na kundi la kazi alioajiriwa katika kipindi cha bajeti ijayo.
Nanok amesema kuwa marupurupu hayo yataongezwa hadi ksh.30,000 katika kipindi cha bajeti cha 2020/2021.
Ameongezea kwamba baraza hilo la magavana limeondoa kesi zote dhidi ya wauguzi hao mahakamani mbali na kuahidi kwamba mishahara yote italipwa mwishoni mwa mwaka huu.

No comments

Powered by Blogger.